... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Uwezo wa Kufanana na Mungu

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

2 Petro 1:3,4 Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.

Listen to the radio broadcast of

Uwezo wa Kufanana na Mungu


Download audio file

Bila shaka kuna siku utajisikia kuwa mshindi kabisa, kuwa juu, Kuna siku zingine utajisikia kama huna nguvu hata kidogo. Labda siku za unyonge ndizo nyingi kulizo siku za ushindi.

Kosa tunalolifanya sisi sote ni kujilinganisha na watu wengine. Kwa sababu kila wakati tunapojilinganisha mara, ni rahisi kuonakama wengine wao hawana siku mbaya. 

Na hii inasababisha tukatishwe tamaa kabisa kwamba hatuna nguvu hata kidogo za kuwa kama Mungu alivyokusudia tuwe siku tulipoumbwa, wala hatuwezi kutimiza yale aliyoyapanga tuyafanye. Lakini ingekuwaje kama ningekwambia kwamba, tayari Mungu ameshakupa yote unayohitaji ili uishi maisha ya kumcha na kufanana naye zaidi na zaidi? 

2 Petro 1:3,4  Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.  Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa. 

Ndani ya Yesu kuna kila kitu kinachohitajika ili uweze kumwishia Mungu katika uchaji unaotakiwa. Ndani ya Yesu unapata uwezo wa kufanana naye zaidi na zaidi. Jamani, ni utajiri mkubwa!  Kwahiyo … acha kujilinganisha na watu wengine, bali uishi katika uweza wa Mungu. 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.