... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Kupekua Maandiko

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favourites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Luke 4:9-12 Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde; na ya kwamba, Mikononi mwao watakuchukua, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

Listen to the radio broadcast of

Kupekua Maandiko


Download audio file

Niliona kikombe cha kunywea chai au kahawa kikiuzwa mtandaoni kikiwa na maandishi mazuri sana, Kusema ukweli nilitamani kukinunua!

Labda ni utani unaohuzunisha kwasababu leo kuna watu wa Mungu wengi, yaani Wakristo wanaishia imani zao kwa jinsi hiyo hiyo ya kuchekecha Maandiko.  Kama vile mchungaji na mwandishi pia aitwaye John Macarthur aliwahi kusema:  Nusu kabisa ya Ukristo umesimikwa juu ya mistari iliyotolewa ndani ya mazingira ya mistari mingine. 

Ni huzuni lakini amesema kweli.  Uwe wazi ndugu, tunachotaka kukifanya wewe na mimi ni kupekua Biblia na kuchekecha mistari inayotupendeza na kuiacha mingine inayosumbua – mfano, kugeuza shavu la pili, kwenda maili ya ziada, kuchukua msalaba wako na kumfuata Yesu … n.k. 

Lakini haiko hivi.  Mimi nafahamu hilo, sisi sote tunalifahamu, lakini je!  Tunalifahamu kwa ndani kabisa? Je!, Tuko tayari kupokea vipengele vinavyotupa changamoto ndani ya Neno la Mungu kama tunavyofurahia vipengele vingine? 

Wakati Yesu alijaribiwa jangwani, Ibilisi na yeye alipekua Maandiko: 

Luke 4:9-12  Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde; na ya kwamba, Mikononi mwao watakuchukua, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.  Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 

Acha tabia ya kupekua na kuichekecha Biblia. 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.